Sunday, June 10, 2012

Kumbe ya Kale Ndo' ya Leo


Ya kale ndo’ ya leo

Wakisema wanaenda Kilaguni,
Kumbe ukweli ni kilabuni?
Eti wazungumziya vyeo,
Na ukweli watetea vyoo!
Wananena wana hoja,
Cha ukweli wanayo haja!
Twaambiwa ni mkutano,
Kumbe ni mtukano?

Kwenda kwa Bunge,
Si kwenda kubonga.
Na kubugia vibonge!
Wanatunyima Unga,
Twalazimika kufunga!

Miswada hawapitishi,
Misaada hawapatiani!
Tukasema Katiba twabadilisha,
Tubadilike na wakati.
Badalake, wakabadilisha wakati!

Ministry kabadilisha majina,
Sasa ni ‘many-strays
Ministers nao, wamekuwa ‘mini-stars’!
Kama sio ‘many stars’!
Justice ni In-justice
Constitution ni Pro-stitution!
Ama kwa hakika
They got our foot in our mouth!
Shame on us and sit on it!
Na same on U n shit on hate!

Kwani uta do?


Martin Okariithi
@2012

No comments:

Post a Comment